Sunday, June 16, 2013

Serikali, UNICEF wazindua program ya redio kufifisha maambukizi ya VVU hadi sifuri



TUME ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) kwa kushirikian na shirika la UNICEF pamoja na kituo cha Clouds Radio mwishoni mwa wiki wamezindua kipindi maalumu cha redio kijulikanacho kama “Shuga” mahsusi kwa vijana kikilenga kuwawezesha  kuongea na kuwasiliana kuhusu jinsi ya kujikinga na maambukizi ya VVU na UKIMWI.
Kamshna wa TACAIDS Bi Faraja Kotta Nyalandu akiashiria uzinduzi wa programu ya Shuga mahsusi kwa kuwalinda vijana na maambukizi ya VVU kupitia Redio Clouds juzi huko Kinondoni, Biafra

Uzinduzi huo ulifanyika katika viwanja vya Biafra, Kinondoni, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

Shuga kinalenga kuchochea maongezi miongoni mwa vijana kuhusu VVU na UKIMWI kwa kutoa burudani na elimu ambayo itakuwa inawaasa kuhusu hatari zinazowakabili kama hawatachukua tahadhari inayofaa

Ni mtiririko wa vipindi 12 ambavyo vitarushwa na redio Claud FM ya Dar es salaam pamoja na ile ya Kitulo FM ya Makete, mkoani Njombe. Lengo ni kufikia ndoto ya kitaifa ya kufuta kabisa kabisa maambukizo ya VVU miongoni mwa watanzania  hadi kufikia sifuri ifikapo mwaka 2015
Mwakilishi Mkazi wa UNICEF nchini Dk.Jama Gulaid akisoma hutoba wakati wa uzinduzi huo

Mgeni wa Heshima katika hafla hiyo—Mwenyekiti Mtendaji wa TACAIDS Dk Fatma Mrisho—ambaye aliwakilishwa na Mkurugenzi wa Ulaghibishi na Habari wa Tume Bw. Jumanne Issango alisema uzinduzi wa Shuga ulikuwa muhimu na umekuja wakati muafaka katika kipindi ambacho maambukizi ya VVU miongoni mwa vijana yalikuwa yanaongezeka.

Kasema, kila siku kuna mambukizi mapya 2,500 miongoni mwa vijana duniani kote, wanne kati ya kumi wanatoka Kusini mwa Jangwa la Sahara (SSA) ambapo ndipo wengi wa vijana hawa wa kike na kiume wanatoka
Baadhi ya wakazi wa Biafra wakifuatilia uzinduzi huo

Mwelekeo kama huo umejionesha Tanzania kwa mujibu wa ushahidi wa hivi karibuni, akasema Dk Jama Gulaid—mwakilishi mkazi wa UNICEF nchini wakati wa hafla hilo iliyohudhuriwa na mamia  ya wakazi waeneo hilo lililo karibu na Chuo Kikuu Huria (OUT).

Programu ya Shuga ni mfano wenye matumaini wa ushirikiano kati ya taasisi za umma, na binafsi kwa kufanya kazi pamoja na vijana ili kuchangia katika jitihada za kupunguza maambukizo mapya ya VU, alisema Dk Jama na kuongeza: Shuga ni kipindi ambacho kitajikita katika kuchochea mabadiliko ya tabia. Ni kipindi kitakachobainisha vichocheo vya mambukizi ya VVU miongoni mwa vijana na kutoa mwangaza wa namna ya kupata huduma za ushauri nasaha, upimaji na matumizi ya kondomu.
Baadhi ya washiriki wa uzinduzi huo

Kwa mujibu wa matokeo mapya kabisa ya Utafiti wa Kitaifa kuhusu mwelekeo wa UKIMWI na Malaria (THMIS, 2012) kumekuwa na kupungua kidogo kwa maambukizi miongoni mwa watanzania wenye umri kati ya miaka 15 na 49. Hii ni kutoka asilimia 7 mwaka  2003 hadi asilimia 5.1 mwaka 2012

Hata hivyo, kwa mujibu wa Dk Mrisho, kiwango cha mambukizi bado kiko juu ikiwa ni takribani ya wastani wa watanzania 80,000 wanaoambukizwa kila mwaka.

“Hakika naamini kwamba ubunifu huu ambao unawaunganisha vijana na wadau wengine katika vita hii ndio unaotakiwa hapa kwetu ili kutuwezesha kufikia lengo la maambukizo sifuri,” alisema Dk Mrisho.
Umma ukifuatilia matukio uwanjani hapo

Mkurugenzi wa Clouds Radio Bw. Joseph Kusaga,alisema ushirikiano huo ulikuwa wa kutia moyo na kuahidi kutumia tasisi yake kuendelea kutoa elimu sahihi na elimishi kwa lengo la kuwasaidia vijana kuwa na afya bora hadi kufikiaa utu uzima
Wageni waalikwa

Naye Bi Faraja Kotta Nyalandu ambaye ni Kamishna wa Tume pamoja na kuwa  balozi wa Shuga akawaataka vijana wasikubali kuuza mechi. Kwa mujibu wa Bi Nyalandu kauli mbiu ya “kijana usiuze mechi” alilenga kuwaasa vijana kuchukua tahadhari wakati wa mahusiano ya kingono.
Bi Vicky Chuwa akimwongoza Mwakilishi wa UNICEF kutoka jukwaani

Uzinduzi huu unaashiria utekelezwaji wa mkakati wa mataifa kadhaa ya kikanda uliosimamiwa na ya UNICEF, Multi-Media Television (MTV) na Kizazi kisichokuwa na UKIMWI wa PEPFAR sasa unaridhiwa katika maudhui ya kitanzania.
Kiduku

0 comments:

Post a Comment