Wednesday, January 29, 2014

AJAAT yazawadia washindi wa makala za kutokomeza unyanyapaa na kutotengwa kwa WAVIU, makundi maalum

    Yumo Akitanda wa CCK
 
Baadhi ya washiriki wa shindano wakimsikiliza kwa makini mmoja wa wasahihishaji wa shindano Bw. Benedict Sichalwe kutoka AJAAT. Kushoto kabisa ni Bw. Kivamwo, mwenyekiti wa AJAAT
DAR ES SALAAM, Januari 25, 200: WAANDISHI wa habari sita kutoka vyombo vya habari nchini wameshinda na kuzawadiwa kutokana na uandishi wa shindano la “KUTOKOMEZA UNYANYAPAA NA KUTOTENGWA WATU WANAOISHI NA VVU PAMOJA NA WALIO KATIKA MAKUNDI MAALUM” lililofanyika kati ya Desemba 20 na 31, mwaka jana.
Mwenyekiti Bw Kivamwo akitoa tathmini ya shindano kwa washiriki kabla ya kukabidhi zawadi
Waadishi walioshinda na majina ya vyombo vya habari wanakofanya kazi katika mabano ni Lucy Ngowi (Tanzania Daima), Harrieth Mandari (The African), Said Mmanga (Changamoto), Richard Makole na Salome Kitomari wote kutoka gazeti la Nipashe. Mwingine ni mwanasiasa machachari ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari Bw. Constantine Akitanda. Bw. Akitanda, kiongozi wa Chama Cha Kijamii (CCK) ameshinda kupitia makala yake aliyotoka katika gazeti la Nipashe  Desemba 28, 2013.
Mshindi kutoka Nipashe Bw.Richard Makore (kushoto) akikabidhiwa zawadi na Bw Perege Gumbo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa AJAAT

Akiwakabisha zawadi  waandishi hao, Mwenyekiti wa AJAAT Simon Kivamwo jana alisema kuwa ushindi wao umetokana na makala walizoandika na kuziwakilisha AJAAT na kupitiwa na waamuzi na kuonekana kuwa bora.
Hafla fupi ya utoaji zawadi kwa waashindi hao ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa AJAAT uliopo Kijitonyama, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam
Alisema, shindano hilo lilihusisha wanahabari 30 kutoka vyombo vya habari mbalimbali nchini waliopewa mafunzo maalum ya siku tatu juu ya uandishi na upashanaji  habari utakaosaidia kutokomeza unyanyapaa na utengwaji wa watu wanaoishi na VVU kwa watu walio katika makundi maalum.
“Hili lilikuwa shindano la papo kwa papo. Baada ya mafunzo yale tuliwaaalika washiriki kuandika makala zenye vigezo vinavyotokana na mafunzo yenyewe. Nawapongeza wale walioitikia mwito,” akasema Bw. Kivamwo
Mshindi kutoka Changamoto, Bw Saidi Mmanga

Shindano hilo lilifuatia mafunzo yalitolewa na Chama cha Waandishi wa Habari za UKIMWI Tanzania (AJAAT), kwa ufadhili wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kupambana na UKIMWI (UNAIDS), yalifunguliwa na Mwakilishi Mkazi wa UNAIDS, Dk. Patrick Brenny, Desemba 17, 2013.
Katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Dr. Brenny alisema vyombo vya habari katika kazi zao za kila siku vina nguvu kubwa ya kuchangia katika kampeni ya kufikia Sifuri Tatu za maambukizo mapya VVU sifuri, vifo sifuri vitokanavyo na UKIMWI na Unyanyapa sifuri kwa watu wanaoishi na VVU ifikapo mwaka 2015.
Lengo la mashindano hayo lilikuwa kuwashindanisha wana habari kuandika  makala zitakazosaidia kutokomeza unyanyapaa na utengwaji wa watu wanaoishi na VVU pamoja na walio katika makundi maalum kama sehemu ya kampeni ya taifa ya kufikia “SIFURI TATU.
Harrieth Mandari wa The African akipokea zawadi kutoka kwa Bw.Gumbo

Umuhimu wa kuyashirikisha makundi  maalum unatokana na hatari kuwa kama wanatengwa na kunyanyapaliwa, watazidi kujificha na kutopima hali zao.
Kuendelea kujificha kwa watu walio katika kundi maalum kunaweza kuongeza maabukizo ya VVU na kufanya kutofikiwa malengo ya SIFURI TATU.
Makundi haya maalumu yaliyo katika  hatari kusababisha kutofikiwa malengo ya kitaifa ya sifuri tatu ni wanaojidunga sindano katika matumizi ya dawa za kulevya, wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja na wenye kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.
Bw Constantine Akitanda wa CCK na Nipashe

Ripoti za viashiria vya Malaria na VVU ya mwaka 2012 imeyataja makundi hayo kuwa na viwango vya juu vya maambukizo ya VVU. Pamoja na kampeni ya taifa ya kukabiliana na maambukizo mapya, kama hatua sahihi za kudhibiti na kukabili kasi ya maambukizo katika makundi haya  hazitachukuliwa, yanaweza yasipatikane mafanikio yaliyokusidiwa.
Bi Salome Kitomari wa Nipashe


Lucy Ngowi wa Tanzania Daima



0 comments:

Post a Comment